Timiza ndoto yetu

Dhamira ya Kuwawezesha Vijana

Kutengeneza Mtandao imara, wenye nguvu na ushawishi ili kuwaleta pamoja vijana na wanawake katika kujenga mtazamo chanya juu ya Mustakabali wao (Mapinduzi ya kifikra) na kuhakikisha mgao sawa wa rasilimali katika maendeleo ya nchi uwe ni haki ya kila raia

Kufikia Jamii

Kushiriki katika shughuli mbalimbali za kujitolea ili kuigusa jamii yenye uhitaji ili kutengeneza na kukuza mazingira ya usawa kwa jamii.

01

Michezo Na Sanaa

Kukuza ubunifu na vipaji kibiashara kwa vijana na wanawake ili kuwa kuwafungulia fursa za kujiajiri.

02

Uezeshaji Kiuchumi

Kujenga uchumi wezeshi na jumuishi kupitia miradi bunifu na ujasiriamali ambayo itawainua na kuongeza hamu au kuchochea jitihada za maendeleo..

03

Tafiti

Kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali tutaendesha tafiti zinazohusu mambo ya vijana na wanawake ili kujenga ufahamu, ubobevu na kuviarifu vyombo vya maamuzi juu ya sera za vijana na wanawake

04

Kujenga Jukwaa La Vijana

Kuanzisha na kujenga mtandao imara wa vijana ambao utakuwa ndio sauti, ushirikishwaji, uwezeshaji wa rasilimali kwa shughuli mbalimbali za vijana

05

Kukuza Matumizi Ya Kidigitali

Kushirikishana katika ubunifu, uvumbuzi na uwezeshaji katika kuleta mapinduzi na kukuza matumizi sahihi ya kidigitali.

06
About
Hukusu Sisi

Maono ya Vijana Wanaoendesha Kesho.

Kuwawezesha vijana kwa ajili ya maendeleo ya usawa bila kujali tofauti zao ili kufikia mabadiliko ya pamoja.

Taifa Letu, Kesho Yetu Movement ni mtandao wa vijana uliopo nchi nzima ambapo unaoendesha vuguvugu la kujitolea ili kuleta mapinduzi ya kifikra katika jamii na unaamini kuwa mgao sawa wa rasilimali za Taifa letu ni haki ya kila raia.

Mtandao huu unaunganisha vijana na kuhimiza ushiriki wao wa moja kwa moja katika fursa mbalimbali ili kuharakisha maenedeleo nchini kote katika sekta za kiuchumi, kijamii, kidijitali na kitamaduni bila kujali dini, itikadi za kisiasa, kabila au ukanda.

Dira/ Maono

Kujenga mtandao imara wenye lengo la kuleta mapinduzi ya kifikra kwa vijana na wanawake.

Jiunge sasa

Misheni

Kutengeneza Mtandao imara, wenye nguvu na ushawishi ili kuwaleta pamoja vijana na wanawake katika kujenga mtazamo chanya juu ya Mustakabali wao (Mapinduzi ya kifikra) na kuhakikisha mgao sawa wa rasilimali katika maendeleo ya nchi uwe ni haki ya kila raia.

Jiunge sasa

Maadili ya Msingi

Utaifa, Uzalendo, Usawa, uwezeshaji, ubunifu, ushirikiano na ujumuishi.

Jiunge sasa
Kanuni zetu

Tk Movement Inazingatia Kanuni Na Sheria Zifuatazo

  • 01Ubaguzi

    Kutojihusisha na ubaguzi wowote wa kikabila, kidini, kikanda, kisiasa nk

  • 02Kuzingatia Kanuni za Kisheria

    Kuzingatia kanuni na sheria za Nchi Kuzingatia sheria na kanuni za jamhuri ya muungano wa Tanzania.

  • 03Ahadi ya Kupinga Chuki

    Kutoshiriki uchochezi Kutojihusisha na uchochezi wa chuki dhidi ya mtu yeyote.

  • 04Matumizi ya Maadili ya Mitandao ya Taasisi

    Matumizi sahihi ya Mitandao ya Taasisi Kutotumia mitandao ya taasisi kwa matumizi binafsi

Work Work